Kwa mujibu wa Kitengo cha Kimataifa cha Shirika la Habari la Hawza, matini ya barua ya Kiongozi Mkuu wa Mapinduzi, Ayatullah Sayyid Mujtaba Husseini Khamenei, kwa Katibu Mkuu wa Muqawama wa Kiislamu wa Kata’ib Sayyid al-Shuhadaa ni kama ifuatavyo:
بسم الله الرحمن الرحیم
Kwa Mheshimiwa Hajj Abu Alaa al-Wala’i (daamat tawfiiqaatukum)
السلام علیکم و رحمة الله و برکاته
Kwa njia hii, tunawasilisha kwako shukrani na tathmini yetu kubwa kwa ajili ya kuonesha kwako hisia za majonzi na rambirambi kwa mnasaba wa kuuawa kishahidi Kiongozi Mkuu wa Mapinduzi ya Kiislamu nchini Iran, Mwenyezi Mungu aitakase roho yake tukufu na kuifanya safi na yenye kutakasika.
Tunamuomba Mola Mtukufu akujalie mafanikio na akupe tawfiqi katika njia ya kuitumikia dini iliyo nyooka ya Uislamu.
Sayyid Mujtaba Hosseini Khamenei
Tarehe 4 Farvardin 1405 Hijria Shamsia
Sambamba na tarehe 4 Shawwal al-Mukarram 1447 Hijria Qamaria

Maoni yako